DIWANI AMWAGA MISAADA UWT KUMUUNGA MKONO RAIS DK. SAMIA

Na MWANDISHI WETU


Mlezi wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Kata za Makongo, Kinondoni  na Bunju, wilayani Kinondoni, jijini Dar es Salaam ambaye ni   Diwani wa Viti Maaumu, Grace Mwashala, amekabidhi msaada  wa wa vitu mbalimbali vyenye thamani y ash. 1,200,000 kwa uongozi wa UWT Kata ya Kinondoni, jijinii Dar es Salaam.

Diwani huyo amekabidhi vitenge 55,kadi za UWT   333 , fedha  ya kufungua akauti  20,000 na  fedha za kuanzia akiba katika akaunti sh. 50,000.

Grace  amesema dhamira ni kuunga mkono jitihada za Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kuwakwamua wanawake kiuchumi  kwani vitu hivyo alivyo kabidhi ni kwaajili ya kuanzisha mradi ambapo fedha itakayopatikana itaingizwa katika akauti ya UWT ya kata hiyo.