MWENYEKITI WA CCM TANGA-TUKO TAYARI KWA UCHAGUZI KUWAGALAGAZA WAPINZANI
Na MWANDISHI WETU
Mwenyekiti wa CCM, Mkoa wa Tanga, Rajab Abdallah, amesema wako tayari kwa uchaguzi wa viongozi wa serikali za mitaa kwani wamejipanga vya kutosha kuwagalagaza wapinzani.
Pia, amewata wananchi wa Tanga kuendelea kujiandikisha katika daftari la kupiga kura, kupata fursa ya kuwachagua viongozi wanao wataka watakao waletea maendeleo.
Mwenyekiti Abdallah ameyasema hayo jijini Tanga, wakati akiendelea na hamasa ya kujiandikisha katika daftari la Kudumu la Wapiga kura.
Amesema Tanga hamasa nikubwa ya kujiandikisha, hivyo wanaimani kuwa itawawezesha kufanya vizuri katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa kupata viongozi wanaotokana na CCM.
MWENYEKITI WA CCM TANGA-TUKO TAYARI KWA UCHAGUZI KUWAGALAGAZA WAPINZANI
Reviewed by Gude Media
on
October 17, 2024
Rating:
Reviewed by Gude Media
on
October 17, 2024
Rating:
