TMDA YAKABIDHI MAGEREZA MWANZA DAWA ZA SH. MILIONI 56
Jeshi la Magereza Mkoa wa Mwanza, limeishukuru Mamlaka ya Dawa na Vifaa tiba Tanzania (TMDA) kwa msaada wa dawa zenye thamani ya sh. Milioni 56.
Akipokea msaada huo kutoka jwa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Said Mtanda, Mkuu wa Magereza Mkoa wa Mwanza ( SACP) Justin Kaziulaya, amesema dawa hizo zitasaidia kwa kiasi kikubwa katika magereza mkoani humo na kuishukuru TMDA kwa msaada huo.
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Said Mtanda, ameishukuru TMDA kwa maaada wa dawa hizo kwa jeshi hilo muhimu.
Meneja wa TMDA Kanda ya Ziwa Mashariki,Sophia Mziray, amesema mamlaka hiyo inatambua umuhimu wa jeshi hilo na kuona umuhimu wa kushirikiana hususan katika sekta ya afya.
TMDA YAKABIDHI MAGEREZA MWANZA DAWA ZA SH. MILIONI 56
Reviewed by Gude Media
on
May 20, 2024
Rating:
Reviewed by Gude Media
on
May 20, 2024
Rating:
