SIMBACHAWENE AZIWEKA MTEGONI WAKALA ZA SERIKALI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa  Umma na Utawala Bora, George Simba Chawene akifungua Mkutano wa Watendaji atendaji Wakuu wa Wakala za Serikali, Dar es Salaam.
Na Mwandishi Wetu

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti  ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, George Simbachawene, amesema haridhishwi na baadhi ya wakala za serikali na kuomba  watendaji wake kujitathimini.

 Aidha  amewataka Watendaji Wakuu  wa wakala hizo  kujitathimini kama wakala wanazoziongoza zimefikia mafanikio ama  wameanza kufanya kazi kwa  maazoea.

Waziri Simbachawene, amesema hayo leo, alipofungua   Mkutano wa Watendaji Wakuu wa Wakala za Serikali, Dar es Salaam, huku akisisitiza, watendaji kufuata madili, miongozo, mifumo na mabadiliko yanayofanyika katika kuleta tija.