DC IRAMBA AWATAKA WATANZANIA KUENZI FALSAFA YA WAASISI WA CCM

 

Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Suleiman Mwenda, akizungumza katika uzinduzi wa maadhimisho ya miaka 47 ya CCM yaliofanyika katika Kata ya Kaselya, wilayani Iramba, mkoani Singida. (Picha na Hemedi Munga).

Na HEMEDI MUNGA

Uzinduzi wa maadhimisho ya  miaka 47 ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) mkoani Singida, umemuibua Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Suleiman Mwenda, kuwataka watanzania kuenzi falsafa za wasisi wa Chama.

Uzinduzi huo umefanyika  katika Kata ya Kaselya,  wilayani  humo  ambapo Mwenda amesema waasisi wa Chama  walikianzisha kwa malengo ya watu kuwa wa wamoja  katika nchi moja.

Ameeleza kuenzi falsafa hiyo ni  watanzania kuendelezaa umoja, mshikamano na upendo katika Taifa lao.

Ameeleza  kwa namna yoyote mwananchi akizunguka Tanzania  lazima  akitazame Chama cha Mapindunzi ambacho kimetengeneza jamii ya watu wanaojitambua, kuheshimiana, kushirikiana na kupendana.

Kuhusu Mwenyekiti wa CCM, Rais  Dk. Samia Suluhu Hassan, Mwenda aliwaomba wananchi  mkoani humo kumchagua  Rais huyo kwa asilimia 100 katika Uchaguzi Mkuu waa mwaka 2025 aendelee kuwa kamisaa wa kuwasimamia wananchi wa Iramba  katika kuwaletea maendeleo.

 Amesema Rais Dk. Samia  ametekeleza kwa kiwango ambacho hakijawahi  kufikiwa na  tangu uhuru wa nchi  kuwaletea maendeleo waananchi wa wiilaya hiyo.

Mwenda  pia aliwataka wananchi   kuhakikisha wanachagua wenye viti wa serikali za mitaa wanaotokana na CCM katika uchaguzi wa serikali za mitaa.

Akizungumzia sekta ya afya, DC Mwenda,  amesema  katika kipindi cha uongozi wa Rais Dk. Samia  wilaya hiyo imezindua  vituo vya afya vipya saba.

Ameeleza lengo la Rais  Dk. Samia na maelhuyo ikiwemo maelekezo ya Ilani ya Chama hicho ni kuhakikisha kila kata inakuwa na  kituo cha afya.

Aliongeza, wameboresha Hospitali ya Wilaya ya Iraamba  ikiwa ni pamoja na kuongeza vifaa tiba  vya kisasa  tofauti na awali ambapo wananchi walilazimaka kufuata huduma hizo mkoani Dodoma.

Ameeleza Zahanati 13  zimejengwa ambapo lengo ni kila kijiji kati ya vijiji 70 vya wilaya hiyo kupata zahanati.

Kuhusu umeme, Mwenda, amesema wilaya hiyo ilikuwa na vijiiji 50 vyenye umeme  lakini sasa   vijiji vyote  70 vimefikiwa   huku vitongoji 184 vinaumeme kati ya vitongoji 390 .

Amesema kuna  miradi 12 mikubwa ya maji inayoendelea kutekelezwa katika wilaya hiyo, hivyo changamoto ya maji haitakuwepo.

Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo, Innocent Msengi, amesema  alisema Baraza la Madiwani lipo salama, halina makundi na limeungana tayari kwa kufanyakazi, hivyo shughuli za maendeleo katika kila kata zinaendelea vizuri.


Katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilayani Iramba mkoani Singida, katikati,  Ephraim Kolimba akimueleza Katibu wa chama hicho mkoa huo, kulia, Lucy Shee uandikishaji wa wanachama wapya kielektroniki, leo katika uzinduzi wa maadhimisho ya kuzaliwa kwa CCM kimkoa kutimizà miaka 47  yaliofanyika katika kata ya Kaselya wilayani Iramba mkoani Singida. (Picha na Hemedi Munga).



Mwenyekiti wa Halmashauri ya  Wilaya ya Iramba Mkoani Singida, Innocent Msengi  akieleza ushirikiano wao na juhudi zake za kupita katika kata  20 za wilaya hiyo kuhamasisha mapato na kufanikiwa kutoka kwenye bajeti ya sh bilioni 1.9 tangu mwaka jana kwa kufikisha bajeti ya sh bilioni 3.3, katika uzinduzi wa maadhimisho ya kuzaliwa kwa CCM kimkoa kutimizà miaka 47  yaliofanyika katika kata ya Kaselya wilayani Iramba mkoani Singida. (Picha na Hemedi Munga)