MKALAMA - SINGIDA
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa Mkoa wa Singida, Martha Mlata amefurahishwa na mafanikio lukiki ambayo Rais Dk. Samia Suluhu Hassan amewaletea wananchi.
Akizungumza na wananchi na wanachama wa chama hicho, Martha amesema Rais Samia ameleta maendeleo makubwa ambayo hayakuwahi kutokea tangu kupatikana uhuru wa nchi hii.
Martha ameyasema hayo wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kijiji cha Kidarafa, Kata ya Mwanga wilayani Mkalama mkoani Singida.
Aidha Martha amewaomba wananchi kuendelea kumuunga mkono Rais Dk. Samia kwasababu amejipambanua kumjali kila mtanzania popote alipo huku akiwaasa kuendelea kuwa watulivu kwa sababu serikali ya CCM inaendelea kutekeleza ilani kwa kishindo.