MWENGE WA UHURU WATEMBELEA MIRADI YA SH. BILIONI 74.5 KINONDONI

Na Mwandishi Wetu

Mwenge wa Uhuru umeendelea na mbio zake mkoani Dar es Salaam, ambapo umeingia wilayani Kinomdoni na kutembelea miradi saba  yenye thamani ya sh. bilioni 74.5.

Akipokea mwenge  huo kutoka kwa Mkuu wa Wilaya ya  Ubungo, Hashim Komba, Mkuu wa Wilaya ya  Kinondoni,  Saad Mtambule, ametaja miradi  hiyo kuwa ni Mradi wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Mkoa wa Dar es Salaam (DAWASA). 

Amesema mradi huo uliopo Mtaa wa Kihonzile Kata Wazo,   umedhaminiwa na Benki ya Dunia na unathamani ya sh. bilioni 71. 

Mtambule, ameeleza  miradi mingine ni klabu ya upingaji rushwa katika Shule ya Msingi Mabwepande, upandaji miti katika Gereza la Wazo na uwekaji jiwe la msingi katika jengo  la wagonjwa  wa nje katika Zahanati ya Mabwepande.

Pia miradi wa  kikundi cha ujasiriamali (KIUWA), kutembelea shughuli za lishe  katika Shule ya Sekondari Daniel Chongolo, na miradi ya usambazaji wa gesi majumbani unaotekelezwa na TPDC.

Mtambule ametaja  mradi mwingine ni ujenzi wa Barabara ya Mkalama Kata ya Ndugumbi yenye urefu wa kilomita 0.8.

“ Mradi mwingine ni uwekaji jiwe la msingi katika  mradi wa ujenzi wa vyumba  12  vya madarasa , matundu 22 ya vyoo katika Shule ya Sekondari Kumbukumbu,”alieleza Mtambule.

Amesema miradi yote hiyo  inajumla ya thamani y ash. bilioni  74 . ambazo zimetolewa na serkali binafi na mapato ya ndani ya  hamashauri hiyo.

Kiongozi wa Mbio za Mwenye wa Uhuru Kitaifa, Abdallah Shaibu Kaimu, alipongeza viongozi wa Wilaya ya hiyo  na watendaji kwa  utekelezaji mzuri wa miradi ya maendeleo.

"Katika miradi huu wa maji wa DAWASA barabara ya Mwenge wa Uhuru, umekagua  nyaraka za ujenzi ziko vizuri. Pia umekagua mradi wenyewe uko vizuri ."alisema Kaimu.

Kaimu  alisitiza uwajibikaji, kupiga vita rushwa, matumizi ya dawa za kulevya, mapambano dhidi ya Maralia, Ukimwi, kuzingatia lishe bora na kutunza mazingira.

Mwenge wa Uhuru tayari umetembelea Wilaya za Temeke, Kigamboni, Ilala, Ubungo ambapo  kesho  utaendelea na mbio zake Wilaya ya Mjini Magharibi, Zanzibar.

MTOTO Azizi Omary (9), akiwa amebeba Mwenge wa Uhuru wakati wa hafla ya kuupokea  kutoka Wilaya ya Ubungo, iliyofanyika katika viwanja vya Shule ya Msingi Mabwepande,  Dar es Salaam. Kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Saad Mtambule. Mtoto huyo aliomba  kikosi cha Wakimbiza Mwenge kuubeba mwenge huo.