Na Mwandishi Wetu
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, amezindua kambi za huduma ya upimaji afya na matibabu bila malipo Afya Check, katika Shule ya Msingi Mbagala Rangi Tatu, wilayani Temeke.
Chalamila amesema kambi hizo zitafanyika katika wilaya zote tano za mkoa wa Dar es Salaam, lengo kuwafikia wananchi 20,000.
Uzinduzi huo umefanyika Mbagala katika Shule ya Msingi Mbagala Rangi Tatu, wilayani huo na kuhudhuriwa na umati wa wananchi kupima afya zao na kupatiwa matibabu.
Chalamila amesema, upimaji afya na matibabu bure utafanyika kwa siku 10 katika wilaya ya Temeke, Kigamboni, Kinondoni, Ubungo na Ilala.
Amesema magonjwa yatakayo husika ni saratani, moyo, shinikizo la damu, Ukimwi, chanjo dhidi ya Uviko 19, chanjo kwa watoto chini ya miaka mitano ambao hawakupata chanjo hiyo au hawakumaliza.