RAIS DK. SAMIA AWASILI NCHINI NAMIBIA KUHUDHURIA MAZISHI YA ALIYEKUWA RAIS WA NCHI HIYO, DK. GEINGOB

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, akiwasili katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Hosea Kutako, Windhoek nchini Namibia kwa ajili ya kuhudhuria mazishi ya aliyekuwa Rais wa Namibia Marehemu Dkt. Hage Geingob, tarehe 23 Februari, 2024. Shughuli za Mazishi za Rais huyo Hayati Dkt. Hage Geingob zitafanyika katika Jiji la Windhoek tarehe 24-25 Februari, 2024.