IRAMBA - SINGIDA
Mkuu wa Mkoa wa Singida, Halima Dendego amewaongoza wananchi wa wilaya ya Iramba kufanya usafi wa mazingira.
Dendego amefanya zoezi hilo leo, katika eneo la dampo liliyopo mjini Kiomboi wilayani hapa mkoani humu.
Akizungumza na wananchi walioshiriki katika usafi huo, amewashukuru wanakinama kwa kuwa mstari wa mbele katika zoezi hilo huku akiwataka viongozi wa soko la mjini hapa kuwajibika kikamilifu.
"Ninataka wananchi wakiowemo viongozi wanaofanya kazi maasa 24 kwa sababu Rais Dk. Samia Suluhu Hassan amaeisha elekeza wanakinama, watu wenyewe mahitaji maalumu na vijana kupata mikopo ya asilima 10 ifikapo julai mwaka huu," amesema.