NA MWANDISHI WETU
Katibu Mkuu wa CCM, Daniel Chongolo, ameongoza Mkutano wa kwanza wa kawaida wa kamati ya uongozi katika Shule ya Uongozi ya Mwalimu Julius Nyerere, mkoani Pwani,
Akitoa taarifa ya mkutano huo, Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM, Itikadi na Uenezi, Sophia Mjema, amesema mkutano huo unajumuisha makatibu wakuu na wawakirishi wa vyama sita Rafiki vya ukombozi kusini mwa Afrika.
Sophia amevitaja Vyama hivyo ni CCM, FRELIMO (Msumbiji), ZANU-PF (Zimbambwe), MPLA (Angola), SWAPO (Namibia) na ANC (Afrika kusini).
Aidha amesema kuwa lengo la mkutano huo ni makatibu wakuu na viongozi wengine na kukagua miundombinu ya Shule ya Uongozi ya Mwalimu Julius Nyerere na kupitia na Kujadili taarifa mbalimbali kuhusu uendeshaji wa chuo hiki.
Pamoja na hayo Sophia, ameeleza malengo ya kuanzishwa kwa shule hiyo ya uongozi ni kuandaa na kufundisha uongozi na uzalendo kwa Makada na wananchi ili kuendelea kujikomboa kiuchumi, kisiasa, kijamii na kifikra, baada ya Ukombozi uliyofanyika wa kuondoa utawala wa kikoloni na kupata uhuru kamili.
Amesema mkutano umeanza Januari 17, 2023 na utamalizika Januari, 19, mwaka huu.