Meya wa Jiji la Dar es Salaam, OMary Kumbilamoto, amewataka wananchi kujitokeza katika kambi maalumu ya Moyo na Figo itakayofanyika Februaru 27 na 28 mwaka huu ambapo vipimo na matibabu itafanyika bure.
Kambi hiyo inafanyika kituo cha DSB Poly Clinic kilichopo Upanga, Mkabala na Msikiti wa Tambaza, Barabara ya Umoja wa Mataifa.
Kambi hiyo imeandaliwa na kituo hicho kwa kushirikiana na Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, ambapo mbali na Moyo na Figo, kutakuwa na madaktari mbalimbali wa magonjwa ya binadamu hususan lishe na watoto na huduma zote zitakuwa ni bure.
UFIKA panda magari ya kwenda Muhimbili, Barabara ya Umoja wa Mataifa, Uliza Msikiti wa Tambaza, mkabala na msikiti huo utaona bango la DSB Poly Clinic.