Ajali za bodaboda kichocheo upasuaji wa nyonga, magoti kwa vijana wa umri mdogo

Na Mwandishi wetu

Madereva wa pikipiki (Bodaboda), wameshauriwa kuzingatia uendeshaji salama wa vyombo hivyo kuepuka ajali ambazo zinasababisha ongezeko la idadi ya watu wanaopasuliwa nyonga na magoti.

Hayo yamesemwa na Daktari Bingwa wa upasuali wa nyonga na magoti wa Taasisi ya Mifupa Muhimbili (MOI), Dk.Violet Lupondo alipozungumza hivi karibuni.

Ameeleza kuwa, ajali za bodaboda zitaongeza idadi ya upasuaji wa kubadilisha nyonga na magoti kwa vijana wa umri mdogo ambao wanapatiwa matibabu hayo kwasasa kutokana na mivunjiko mibaya ya nyonga na magoti. 

Sababu zingine kwa vijana yanayoweza letea kubadilisha nyonga , yanatokana na magonjwa  kama Rhematoid Athritis,  haemophilia  , sickle  cell na avascular necrosis  ( secondary degenerative disease). ambapo magonjwa hayo  huanza katika  umri mdogo

Dk.Violet alitaja sababu kubwa kwa sasa za  ubadishaji wa nyonga na magoti ni uchakavu ambao unaambatana na umri mkubwa ( primary degeretive joint disease), hali inayotokea zaidi  kwa wazee.

Aliieleza kuwa matatizo haya yapo zaidi kwa watu wazima wanawake na wanaume.

Dk.Violet aliongeza kuwa, kutambua chazo mapema (screening) na kupata tiba mapema, itapunguza ubadilishaji wa nyonga na magoti mapema.

Ukigundulika mapema kuna njia mbadala kama kurekebisha matege, na knocked knee, lakini pia kuna dawa za kupunguza  kasi ya uchakavu hasa kwa magonjwa haya ya vijana niliyotaja hapo awali,  kupunguza uzito na  kufanya mazoezi inasaidia kuondokana changamoto za magoti na nyonga

Amefafanua kuwa, matatizo haya yakigundulika  mapema na kupata tiba inapunguza  kasi ya uchakavu .  Lakini wanaendelea kuongeza jitihada  za kutibu  vijana hao wa boda boda wanaopata mivunjiko mibaya kutokana  ajali.

Ameshauri kuongeza jitihada madhubuti za kudhibiti ajali za bodaboda hususani vijana   Ili kuokoa maisha yao na hatari hiyo ya kufanyiwa upasuaji wa nyonga na magoti wakiwa na umri mdogo, kwani uwezekano wa kurudiwa uko juu, pia inahitaji  vifaa vya marudio na vina  gharama kubwa.

Daktari Bingwa wa upasuali wa nyonga na magoti wa Taasisi ya Mifupa Muhimbili (MOI), Dk.Violet Lupondo.