WANANCHI MABWEPANDE WAMPIGIA SALUTI RAIS DK. SAMIA KUMALIZA MGOGORO WA ARDHI ULIODUMU KWA MIAKA 20


Diwani wa Kata ya Mabwepande, Kinondoni, Mhajilina Kassim 'Obama', akizungumza na wananchi wa kata hiyo kuhitimisha mgogoro uliodumu kwa miaka 20 baina yao na Shirika la Maedeleo ya Jiji la Dar es Salaam (DDC), leo. (Na Mpigapicha Wetu).

 

MKURUGENZI wa Shirika la Maendeleo ya Jiji la Dar es Salaam (DDC), Paulo Mhache (kulia) akizungumza a wananchi wa Kata  ya Mabwepande, baada ya kikao cha kuhitimisha  mgogoro uliodumu kwa miaka 20 baina ya shirika hilo na wananchi haoleo. (Na Mpigapicha Wetu).



Na Mwandishi Wetu

 Hatimaye  wananchi wa Kata ya Mabwepande  wameridhia  Shirika la Maendeleo ya Jiji la Dar es Salam (DDC), kupima maeneo yao na kuwekewa mawe maalumu hatua inayohitimisha  kuhitimisha mgogoro  uliodumu kwa miaka zaidi ya 20.

Jana kimefanyika  kikao kilichowakutanisha wananchi hao  uongozi wa DDC na Diwani wa Kata ya Mabwepande, wilayani Kinondoni,  Mhajilina  Kassim .

Diwani  Obama, amewataka  wananchi hao kuridhia hatua hiyo  na  kuhitimisha mgogoro  huo  ambao amesema unakwamisha maendeleo yao.

“Kwa niaba ya wananchi wa Mbwepande , ninamshukuru   Rais Dk. Samia Suluhu Hassan  kwa kuteua viongozi  wasikivu hatimaye tumehitimisha mgogoro huu katika kipindi cha uongozi wake.

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Daniel Chongolo, MKuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Amos Makalla, Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Godwin Gondwe, Mbunge wa Jimbo la Kawe Dk.  Josephat  Gwajima wame saidia kufikia hatua hii,”amesema.

Ameeleza ataendelea kuwatetea wananchi wake kuhakikisha kila mmoja anapata haki yake kwani hakuna mvamizi wa ardhi katika eneo hilo.

“Hapa hakuna mwananchi mvamizi  bali hawa ni wananchi wanyonge  waliotapeliwa na kuuziwa maeneo na baadhi ya watu. Na natoa onyo wale wote wanaoingia katika kata  hii kutapeli ardhi  huu siyo wakati wao,” amesema Obama

Mkurugenzi wa DDC,  Paulo Mhache, alisema  hakuna mwananchi katika eneo hilo ambaye nyumba yake itavunjwa.

“Lengo letu ni kurasimisha eneo hili la Mabwepande. Kuhakikisha linapimwa na kila mwananchi apate hati itakayosaidia kutambulika rasmi,”amesema Mhache.

Amesema DDC ndiyo mmiliki wa eneo hilo  na  ana hati halisi lakini ni  shirika  hilo ni  mali ya serikali hivyo haliwezi kuwaumiza wananchi hao hivyo kuwataka kuwa watulivu.

“Tulikubaliana gharama za upimaji ardhi kila mwananchi ziwe sh. 8500 lakini diwni wenu aliomba tupunguze hadi  sh. 6500 kwa mita moja ya mraba,”alieleza.

Ameeleza kwa kutambua  hali za maisha fedha hiyo  haitalipwa kwa mkupuo bali italipa kwanza asilimia 10 na  kisha itakuwa ikilipwa kidogo kidogo.

Ameaasa  wananchi kuamini  ardhi ni maisha hivyo wasikubari kuchochewa,  badala yake kila mtu aangalie tija kwa manufaa yake na familia yake.

Wananchi  wameshukuru kwa hatua iliyofikiwa na kumpongeza Rais Dk. Samia,  kuhitimisha mgogoro huo waliodai kwa kipindi kirefu uliwafanya wajione wanyonge.

Amina Abdallah, mkazi wa eneo la  Mwendo kasi katika kata hiyo, amemshukuru Rais Dk. Samia  na kushauri malipo ya upimaji kupunguzwa zaidi kwani wananchi wengi katika eneo  hilo ni wanyonge.

“Tunaomba tupunguziwe gharama ya upimaji  kwani wengi hatuna kipato kikubwa,”amesema

Agosti  10 mwaka huu Mkuu wa Mkoa  wa Dar es Salaam, Amos Makalla aliingilia kati mgogoro huo unaohusisha heka  6000 za DDC na Shirika la Hifadhi ya Jamii (NSSF), ambazo zilivamiwa

Makalla alieleza  eneo hilo lirasimishwe na kupima viwanja na wananchi kununua viwanja hivyo.