MATEMBEZI KUMPONGEZA RAIS DK. SAMIA KULINDIMA NCHI NZIMA

Na Mwandishi Wetu

Waziri MKuu Kassim Majaliwa, anatarajiwa kuzindua matembezi maalumu ya kumpongeza Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, yatakayofanyika nchi nzima.

Matembezi hayo yaliyoandaliwa na Bulding   Natonal Consensus  Foundation (BNC- Tujenge  Mwafaka wa Kitaifa)  ya hapa nchini yana lenga kumpongeza Rais  Dk. Samia kwa utendaji wake, kuendeleza  amani, umoja, mshikammano, mwafaka wa kitaifa na kuanzisha  majadiliano ya katiba mpya na tume huru ya uchaguzi.

Akizungumza na waandishi wa habari, jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa BMC,  Abdallah  Hamis, alisema matembezi hayo yatafanyika katika  mikoa yote nchini.

“Tutangaza rasmi siku ya kuanza  kufanyika  kwa matembezi haya, mahari yatakapozinduliwa. Tunatarajia yatazinduliwa na  Waziri Mkuu  Kassim Majaliwa,”amesema.

Amesema BNC  imeamua  kuja na matembezi hayo kutokana na utendaji uliotukuka wa Rais Dk. Samia, hasa kuleta utengamano katika taifa, kasi ya maendeleo ya kiuchumi na uongozi imara.

Hamis amesema  matembezi hayo yanatarajiwa kupokelewa na Rais Dk. Samia.

Naye Katibu MKuu wa BNC,  Ujamis Katanga, amesema taasisi hiyo ni changa lakini yenye maono ya kushiriana na jamii yote ya Tanzania bila kujali dini, ukabila, tofauti za kisiasa  pamoja na kushirikiana na serikali kutangaza maendeleo.

Kwa upande wa  viongozi wa  madhehebu mbalimbali ya dini nchini, walipongeza Rais Dk. Samia, kwa  kubuni miradi mipya, kuendeleza miradi iliyoanzishwa na watangulizi wake pamoja na kufungua fursa za kiuchumi kimataifa.

Mchungaji Mstaafu wa  Kanisa la Angilikana  Dayosisi ya Tabora, Dk. Isaya Mugaragu, amesema  kazi kubwa iliyofanywa na Rais Dk. Samia, imevuta hata mataifa makubwa kutafuta  fursa hapa nchini.

Mchungaji wa Kanisa la The Apostilic Ministry Tanzania, Baraka Chihamba, aliomba kuimarishwa kwa amani, mshikamano na utulivu.

Sheikh Abdulah Mohammed Said ,  Tasisi ya Wananyota, Kufundisha na Kuhifadhisha Quraan, alisisitiza Watanzania kulinda amani kwa gharama yoyote  na kumpongeza Rais Dk. Samia kwa kusimamia misingi hiyo.