CHALAMILA ATANGAZA MKAKATI KABAMBE WA KUHAKIKI FUKWE KUKOMESHA MAGENDO

Na Mwandishi Wetu

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert  Chalamila,  ametangaza mkakati kabambe wa kuhakiki fukwe  ikiwa ni hatua ya kukomesha kushamiri kwa biashara halamu hususan magedo na magenge ya uhalifu

Ameyasema hayo Dar es Salaam, alipozindua  kampeni ya  usafi endelevu wa ufukwe wa Ununio, wilayani Kinondoni, iliyoandaliwa na Taasisi ya Women  Impact Sustainable Enveronment Foundation (WISE) na kuhitimisha ziara yake wilayani humo.

Amesema  moja ya mkakati ambao  mkoa wa Dar es Salaam utatekeleza ni   kuhakiki fukwe zote na kuangalia tija zake.

“Tunafukwe kutoka Pemba Mnazi Wilaya ya Kigamboni hadi mpaka  wa Wilaya ya Kinondoni na Bagamoyo mkoani Pwani. Fukwe nyingi zimekuwa ni malango ya magendo mengi yanayotoka  upande wa pili,”ameeleza Chalamila.

Chalamila amesema magendo hayo yanayoshamiri ni  kutoka  Zanzibar, Comoro na visiwa vya Anjuan.

“Fukwe hizi zimekuwa malango makubwa ya ukwepaji kodi ambayo Tanzania  inngenufaika na fedha hizo katika miradi mikubwa ya maendeleo na  yenye tija,” amebainisha mkuu wa mkoa.

Ameeleza imebainika fukwe nyingi mkoani humo zimegeuka kuwa vichaka na kimbilio kubwa la magenge  ya uhalifu, hivyo  mkakati huo unalenga pia kusambaratisha magenge hayo. 

“Hatua hii ya tasisi ya Wise  kuzindua kampeni  endelevu ya usafi wa ufukwe wa Ununio ni muhimu  wakati huu tunapoanza kutekeleza mkakati wetu huo,”amebainisha.

Pia Chalamila alisema moja ya mambo yaliyobainika ni kukithiri kwa uchafu wa chupa  za vinywaji  ambazo haziwezi kuchakatwa.

“Tutakaa na Baraza la Taifa la  Usimamizi wa Mazingira (NEMC) na watengenezaji wa bidhaa hizi. Watengeneze  vifungashio   vinavyo weza kuchakatwa.

 Ikumbukwe hivi sasa  tuko katika hatua za kubadili hata mfumo wa dampo letu la Pugu Kinyamwezi  badala ya kulundika taka   Rais Dk. Samia Suluhu Hassan ametuelekeza  taka hizo ziwe zinachakatwa upya,”ameeleza Chalamila.

Awali Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Saad Mtambule, amesema wilaya hiyo inafukwe zenye urefu wa  kilomita 47, ambazo zingetumika vyema zingekuwa kivutio  na uwekezaji mkubwa  wenye tija.

“Ni maeneo ambayo ni utajiri mkubwa. Kama tutautumia vizuri kuendanna na ajenda ya Rais Dk. Samia ya Tanzania The  Royal tour, tungekuwa na uwekezaji mkubwa hapa,”alisema Mtambule.

Awali MKurugenzi wa Taasisi ya Wise, Dorica  Mwanji,  amesema kampeni hiyo ya Ununio Sustainable Shores, ni endelevu na ina lenga kurejesha hadhi ya usukwe huo.

“Kampeni hii inaweeza kuleta athari chanya za mabadiliko ya tabia nchi. Sote tunajua shida ya mabadiliko ya tabia nchi ambayo ni  mafurik, ongezeko la joto duniani , ukame na mengine mengi,”amesema Dorica.

Dorica amesema Wise, itaendelea kufanya usafi katika ufukwe huo  kuongeza uwekezaji,  kipato cha wananchi na kukuza bishara.