MADIWANI KINONDONI WABARIKI BAJETI YA SH. BILIONI 149.4



Na MWANDISHI WETU

BARAZA la Madiwani la Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni, mkoani Dar es Salaam, limeridhia   na kupitisha makadirio ya bajeti ya sh. bilioni  149.4. kwa mwaka wa fedha 2024/25.

Akizungumza katika kikao cha baraza hilo, Meya wa Manispaa hiyo, Songoro Mnyonge, mesema bajeti hiyo  imejikita kwa kiasi kikubwa katika miradi ya maendeleo  na kutekeleza maelekezo ya serikali ya kujitegemea.

 Meya Mnyonge, amesema,  kiasi cha sh. bilioni  75.2 ni ruzuku kutoka Serikali Kuu na sh. bilioni  74.2 ni mapato ya ndani  ya halmashauri.

“Bajeti hii  inathibitisha  Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni inaendelea kujijengea uwezo wa kujitegemea. Hayo ndiyo malengo ya serikali kuzitaka  halmashauri kujitegemea,”amesema.

Alibainisha,  manispaa hiyo  imekuwa mstari wa mbele kukusanya kodi hivyo bajeti yake kupunguza   utegemezi kutoka serikali kuu. 

“Mapato ya ndani yamechangia kwa  sh. bilioni 74.2 katika bajeti hii  sawa na asilimia 49. Serikali kuu imechangia katika bajeti hii  sh. bilioni 75.2  sawa na asilimia 50. Hivyo  tofauti ni ndogo  ya pato la ndani na ruzuku ya fedha kutoka serikali kuu,”amebainisha Meya Mnyonge.

Kwa upande wa Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo, Khanifa  Suleiman, ameilishukuru  baraza hilo kupitisha bajeti hiyo  na kuomba ushirikiano zaidi kwa madiwani hao katika kuijenga halmashauri hiyo