HALMASHAURI YA IGUNGA NA MSD KUENDELEA KUSHIRIKIANA KUTOA HUDUMA BORA KWA WANANCHI

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya Igunga, Selwa Hamid.

IGUNGA - TABORA

MKURUGENZI Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Igunga mkoani Tabora, Selwa Hamid kwa kushirikiana na Meneja wa Kanda ya Tabora wa Bohari ya Dawa (MSD),  Rashid Omar wameahidi utayari wa kuendelea kutoa huduma bora kwa wananchi.

Viongozi hao wametoa ahadi hiyo,  leo  wakati wa kikao kazi kati ya Timu ya Usimamizi wa huduma za afya wilaya (CHMT) na Bohari ya Dawa  ya kanda hiyo inayohusisha mikoa ya Tabora, Kigoma na Katavi  katika hospitali ya wilaya hiyo mjini hapa.

Akizungumza katika kikao hicho Mkurugenzi huyo, Selwa amesema  wanaweza kufikia lengo hilo ikiwa wataendelea kudumisha utayari ambao wanaamini utawawezesha kufikia mafanikio.

Pia,  amewataka wiongozi na watendaji hao kuendelea  kujitathimini na kufanya kazi kwa kuzingatia  ubora na viwango stahiki.